WATOTO WALEMAVU WAIOMBA SERIKALI KUBORESHA HUDUMA ZAO SHULENI
 
     Na Fabiola Nassib wa HEAR MY VOICE-Arusha   Watoto wenye walemavu waishio mkoani Arusha wameililia serikali juu ya   kuboresha mfumo wa elimu hasa sekondari unaowatenga hali inayowafanya   kukata tamaa ya kuthamini elimu.   Wakiongea na HEAR MY VOICE ilipotembelea shule ya msingi Meru kwa   niaba ya wanafunzi wenzake wenye ulemavu wa aina tofauti tofauti   Brenda Honest mwenye ulemavu wa kutosikia (KIZIWI) alisema kuwa  mfumo wa elimu   hasa wa shule za sekondari hau wajali wala kuthamini walemavu kama wao.    Brenda aliendelea kusema kusema kuwa ingawa wao ni walemavu lakini jamii  itambue kuwa ulemavu huo hawakuuchagua hivyo ameiomba serikali na  jamii yote kwa ujumla kuwasaidia kwa kuwasapoti katika mambo mbali  mbali zitakazowawezesha kujitegemea hapo baadae na siyo kuwa tegemezi  siku zote za maisha yao.   Akitolea mfano mambo wanayohitaji kuungwa mkono Brenda alisema kuwa   mfumo wa elimu hasa katika shule za sekondari na kuendelea, haijawapa   kipaumbele walemavu hasa w...
 
