SIMULIZI YA KWELI
Nililazimika kulala kwenye mitaro ili niweze kuiona kesho Miaka takribani saba iliyopita kwenye mtaa fulani hapa Njombe katika usiku wa giza zito uliofunikwa na baridi kali iliyochangamana na ukungu, wapo vijana kadhaa wamelala chini ya mitaro, wamesogeleana karibu ili angalau wapate joto katika miili yao. Mashuka yao ni maboksi yaliyotolewa vitu vya thamani na kutupwa jalalani. Kati ya vijana hawa ambao wamelala chini ya moja ya mitaro ya mji huu wa Njombe yupo kijana aitwaye John Mwingira ambaye kabla ya miaka saba iliyopita alikuwa akiishi nyumbani kwao Ifakara, wilayani Kilombero mkoani Morogoro. Huko alikuwa akiishi na wazazi wake wote wawili, lakini baadaye wazazi wake waliachana kufuatia kutokuwepo maelewano baina yao. Baba yake akahamia Njombe na mama yake akabakia Ifakara. “Baada ya wazazi wangu kuachana maisha yalikuwa magumu pale nyumbani Ifakara hivyo mama akanishauri nimfuate baba hapa Njombe, nilifika Njombe na kuonana na baba yangu am...



Comments
Post a Comment