TUWASADIE WATOTO YATIMA NA WATOTO WA MITAANI
                                              Hiki ndicho kitanda cha mtoto huyu
                                              Kwa watoto hawa popote ni kitanda
 Wapo watoto wengi ambao wanaishi maisha ya shida na taabu nyingi, wengi
 wakiwa wameondokewa na wazazi wao (wamefiwa na wazazi wao). Ni kweli 
kuwa serikali ina jukumu la kuwaangalia watoto hawa. Sisi
 wanajamii pia tuna majukumu ya kuwasaidia watoto hawa. Tukijitahidi 
kupunguza matumizi ya anasa tukachangia kila mwenye uwezo kidogo kidogo 
hata elfu moja kwa mwezi kwa wale walioajiriwa na hata wafanyabiashara 
tungeweze kutatua tatizo hili tukishirikiana na serikali. Kuna vituo 
vingi vinavyolea hawa watoto ila vinakosa uungwaji mkono kutoka kwa 
wanajamii, kwa hicho kidogo ulichojaliwa na Mungu unaweza okoa maisha ya
 mtoto walau mmoja. Mother Teresa alipata kusema "Kama huwezi kusaidia 
mamia ya watu, saidia hata mmoja"
Naamini jambo hili linawezekana kwa wote wenye imani na uchungu. Fikiri, Chukua hatua, Inawezekana.
Naamini jambo hili linawezekana kwa wote wenye imani na uchungu. Fikiri, Chukua hatua, Inawezekana.

Comments
Post a Comment