UENEZWAJI WA TAARIFA ZA ULEMAVUNI HATUA MUHIMU KWA JAMII DHIDI YA WALEMAVU..
Matukio katika ziara ya mtandao wa Thehabari.com kuangalia huduma za msingi kwa watu wenye ulemavu na uenezwaji wa taarifa juu ya Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Walemavu wilayani Arumeru kwa ufadhili wa ICD
Kikundi
 cha Wanapambazuko Klabu cha Shule ya Msingi Iliboru wilayani Arumeru, 
kikiwa katika picha ya pamoja. Kikundi hichi hufanya hamasa na 
kuelimisha jamii juu ya haki anuai za watoto wenye ulemavu eneo hilo 
ikiwa ni juhudi za ICD.
Bi.
 Vick Kimaro ambaye ni mmoja wa viongozi wawakilishi wa watu wenye 
ulemavu wilayani Arumeru, akionesha nakala ya chapisho lililoandaliwa na
 Kituo cha Habari Kuhusu Ulemavu linalounadi Mkataba wa Kimataifa wa 
Haki za Watu wenye Ulemavu alipozungumza na mwandishi wa mtandao huu 
(hayupo pichani).
Mwalimu
 Mkuu wa Kituo cha Wanafunzi wenye Ulemavu, Shule ya Msingi Naurei 
wilayani Arumeru, Tuzie Mtenga akizungumza na mtandao wa Thehabari.com 
kufafanua shughuli anuai za kituo hicho juzi
Mwalimu
 Mratibu wa Kituo cha Walemavu cha Shule ya Msingi Iliboru, Loitusho 
Yamat akifafanua jambo kwenye mahojiano na mtandao wa Thehabari.com jana
 wilayani Arumeru
Baadhi ya wanafunzi wa darasa la nne (viziwi) katika Kituo cha Walemavu cha Shule ya Msingi Iliboru wakiandika darasani
Mwanafunzi
 Richard Kisanga (18) wa Kituo cha Walemavu cha Shule ya Msingi Naurei 
ya wilayani Arumeru akinakili hesabu kama alivyopewa maelekezo na 
mwalimu wake
Baadhi
 ya walimu waliopo katika mafunzo ya vitendo katika Kituo cha Walemavu 
cha Shule ya Msingi Iliboru wakifundisha darasa la saba
Mmoja
 wa wanafunzi wenye ulemavu (kiziwi), Shule ya Msingi Iliboru  akiandika
 darasani kama alivyokutwa na mpiga picha wa Thehabari.com
Comments
Post a Comment