HIZI NDIZO GHARAMA NA ADHA ZA KUZALIWA MLEMAVU TANZANIA
            
Mtoto Alewis akiwa na mama yake Roswita Mhagama katika ofisi za Mwananchi. Picha na Daria Erasto
 
            
    Na Daria Erasto, Mwananchi
 
Grace aliiambia Mwananchi  kuwa 
amejikuta kwenye hali ya mateso na uchungu mwingi baada ya familia yake,
 hususan mume wake, Erick Mwakyusa kumtelekeza kwa kile alichodai kuwa 
hana haja na watoto walioungana.
Alisema Erick na ndugu zake walimkataa kwa sababu katika ukoo wao haijawahi kuzaliwa mtu wa jinsi ile.
Ashukuriwe Mungu kwa msaada wa wauguzi na 
madaktari wa Hospitali ya Uyole, Hospitali ya Rufaaa Mbeya na Hospitali 
ya Taifa Muhimbili sasa watoto hao wamepata fursa ya kupelekwa India ili
 kufanyiwa upasuaji wa kutenganishwa.
Hali si tofauti kwa Alewis Mhagama (7), mlemavu wa viungo vya mikono na miguu anayetokea kijiji cha Mlimba, Ifakara Mkoani Morogoro. Ukimwangalia na kumsikiliza mtoto huyo utagundua kuwa ni mwerevu na mchangamfu wa hali ya juu.
Lakini, kwa undani Alewis anakabiliwa na upweke kwa kukosa mapenzi ya baba yake mzazi pamoja na ndugu za baba yake, kwani pamoja na kuishi kijiji kimoja, baba yake alimkataa mara baada ya kuzaliwa.
 Kwa maelezo ya mama  mzazi wa Alewis,  Roswita 
Mhagama anasema mwanaye  alizaliwa na ulemavu wa viungo vya mikono  na 
miguu mwaka 2007 kijijini Mlimba.
Baada ya kuzaliwa baba Alewis alimkataa mtoto huyo na kumwita laana na mikosi katika familia.
Roswita anasema alifukuzwa na ndugu wa mwanaume 
huyo na kumwambia kuwa ana laana na dhambi  ndiyo maana amezaa mtoto 
anayefanana na chura. Anasema amemlea mtoto wake huyo kwa mateso 
makubwa,kwani kutokana na ulemavu alionao Alewis amekuwa tegemezi kwa 
mambo mengi hivyo hutumia muda wake mwingi na kumfanya ashindwe kufanya 
 kwa umakini shughuli zake za kilimo na upikaji pombe za kienyeji 
alizokuwa anafanya awali ili kujipatia kipato.
                
              
“Kwa kweli hali ya maisha yangu imebadilika tangu nipate mtoto huyu,pamoja na kwamba nimekosa usaidizi, lakini pia nakosa muda wa kufanya shughuli zangu zingine kwa sababu Alewis anakuwa anahitaji uangalizi muda wote,” anasema.
Anaongeza kuwa hali hiyo imefanya kipato cha familia yake 
kushuka zaidi, kwani tayari ana watoto wengine watatu ambao baba yao 
alifariki naye ndiye anayewasomesha. “Hivi ninavyoongea nawe, mwanangu 
anayefuatana na Alewis kuzaliwa ambaye yuko kidato cha tatu sasa 
alisimamishwa shule kutokana na kutolipa ada,” anaeleza.
Anasema kutokana na maisha duni aliyonayo 
ameshidwa kumpatia mwanae baiskeli ya miguu mitatu ili kumrahisishia 
katika kutembea, hivyo hulazimika kumbeba mgongoni kila anapotaka 
kwenda.
Maisha ya Alewis
Kwa sasa Alewis amefikisha umri wa kwenda shule na
 kutokana na kufundishwa na kaka yake nyumbani anajua kusoma  baadhi ya 
herufi na maneno kama mama, baba na dada.
Hata hivyo, kikwazo kikubwa kilichopo ni upatikanaji wa shule itakayomfaa kulingana na hali yake ya ulemavu.
Nilipomuuliza anataka kuwa nani Alewis alijibu kuwa akiwa mkubwa anataka kuwa daktari na tayari anajua kusoma kwani kaka yake aliyemtaja kwa jina moja la Jumbe huwa anamfundisha akiwa nyumbani.
“Najua kusoma mimi, kaka Jumbe akitoka shule ananifundisha mama, baba, dada na kaka,” anasema Alewis.
Kwa upande wake, Roswita anasema mwaka jana alikwenda Shule ya Msingi Viwanja Sitini iliyoko Ifakara kumwandikisha mtoto wake, lakini walimu wa shule hiyo walimwambia shuleni hapo hakuna nafasi ya kusoma mwanae Alewis kutokana na hali yake.
Alisema alielekezwa kwenda katika shule nyingine huko Ifakara ambayo huhudumia watoto wenye mtindio wa ubongo, lakini nako alipofika, walimu wa shule hiyo walimwambia hiyo ni shule maalumu kwa watoto wenye ulemavu wa akili na lewis hana tatizo hilo.
“Alewis ana hamu ya kwenda shule, na  hapa alipo 
anajua kusoma na kuandika baadhi ya maneno, tatizo hajapata shule, ndio 
maana naomba msaada wa jinsi ya kupata shule ya watoto kama huyu”, 
anasema Roswita.
Baada ya kutafuta shule bila mafanikio huko Ifakara, Roswita anasema amekuja Dar es Salaam ili kupata msaada wa kutafutiwa shule mtoto wake huyo.
Katika pilika pilika hizo amefanikiwa kupata shule iliyokubali kumpokea Alewis ili awaeze kuanza shule ya awali.
Shule hiyo inaitwa St. Bernard iliyoko Mbezi Kibamba, lakini kikwazo kingine ni kuwa shule hiyo haina bweni, hivyo itamlazimu yeye (Roswita) kumpeleka Alewis shule na kumrudisha kila siku.
                
              
Kitu ambacho pia ni kigumu kwani Dar es Salaam amekaribishwa na ndugu yake anayeishi Kimara na si mkazi.
Wito wake kwa jamii
Shule hiyo inaitwa St. Bernard iliyoko Mbezi Kibamba, lakini kikwazo kingine ni kuwa shule hiyo haina bweni, hivyo itamlazimu yeye (Roswita) kumpeleka Alewis shule na kumrudisha kila siku.
Kitu ambacho pia ni kigumu kwani Dar es Salaam amekaribishwa na ndugu yake anayeishi Kimara na si mkazi.
Kikwazo kingine ni ada, kwani shuleni hapo 
anatakiwa kulipa Sh 300,000 kwa muhula, kiasi ambacho ni kikubwa mno 
ukilinganisha na kipato chake.
Wito wake kwa jamii
 Roswita anawataka wanajamii kuachana na dhana 
potofu juu ya ulemavu,anawaomba wasiwatenge  bali wawapokee na 
kuwafariji ili nao wahisi ni watu wa kawaida ndani ya jamii.
Anawaomba wasamaria wema kumsaidia mtoto wake 
kupata shule ya walemavu ya gharama nafuu na pia ikiwezekana wamsaidia  
baiskeli ili naye aweze kutimiza ndoto yake ya kupata elimu.
Kwa kumsaidia Tumia namba 0716 676665
Comments
Post a Comment