TATIZO SUGU
     MAZINGIRA MAGUMU YA KUJIFUNZIA NI CHANZO CHA UTORO KWA WANAFUNZI WENYE WALEMAVU WILAYANI NAMTUMBO.                                    Wanafunzi     walemavu wa akili shule ya msingi Namtumbo wakiwa ofisi ya walimu.Wanafunzi     hawa hawana darasa maalumu la kusomea kwani wakati mwingine huchuliwa na     mwalimu wao na kuwapeleka nyumbani kwake ili kuwapatia chai na     kuwafundishia nyumbani kwake. Ukosefu wa chakula na madarasa ya kusomea kwa     wanafunzi walemavu umesababisha wanafunzi hawa kuwa na mahudhurio madogo na     wengine kutokuhudhuria kabisa.             Mwalimu wa kitengo maalumu cha shule ya msingi Namtumbo Bw  Lezile   Kampango  amesema changamoto kubwa katika kituo hicho pekee cha   wanafunzi wenye ulemavu wa akili wilayani namtumbo ni ukosefu wa   chakula,vifaa vya kufundishia, madarasa na walimu.   “Watoto kama hawa hawawezi kusoma   bila chakula, kwani mwanafunzi akihisi njaa tu anatoka nje na kurudi kwao   bila hata ya kuuliza, gari ikipita wote wana...