Posts

MTOTO ANUSURIKA KUUAWA... WAZAZI HAKUNA MTOTO ANAYEPENDA KUZALIWA AKIWA MLEMAVU.....

Image
BAADHI YA WATU WAMEKUWA NA MITAZAMO HASI DHIDI YA WATOTO WANAOZALIWA NA ULEMAVU WA AINA MBALIMBALI, NA HICHA NI CHANZO CHA NDOA NYINGI KUVUNJIKA, HAKUNA MTOTO ANAYEPENDA KUZALIWA MLEMAVU, WALA MAMA ANAYEPENDA KUJIFUNGUA MTOTO MLEMAVU ILA YOTE NI MIPANGO YA MUNGU WETU AMBAYE NDIYE MUUMBAJI, SIO MKOSI WALA LAANA KUZAA MTOTO MLEMAVU... Mkazi  wa Kawe, Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam,  Betty Mwani (25) amewaomba Watanzania na mashirika  yasiyo ya kiserikali kumsaidia  mahitaji  mbalimbali mwanaye Saraphina Huruma Msaka (7) (pichani) ambaye ni mlemavu aliyenusurika kuuawa. Akizungumza hivi karibuni nyumbani  kwa dada yake, Kawe anakoishi, Mwani alisema kwamba mwanaye alitaka kuuawa kijijini kwao kutokana na imani za baadhi ya watu kuwa katika ukoo wao mtoto kuzaliwa na ulemavu ni mkosi. Hata hivyo, Mwami alisema aliweza kuondoka na kuja jijini ambako mtoto wake anakabiliwa na matatizo mengi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa baiskeli ya magurudumu...

AJIRA KWA WATOTO MAJUMBANI ZIKOMESHWE: ILO

Image
Ajira kwa watoto haifai. ILO Kufua nguo, kuteka maji, kulea watoto wenzao na hata kulea wazee, ni majukumu ambayo Shirika la kazi duniani, ILO limetaja katika ripoti yake kuwa yanakabili watoto walioajiriwa majumbani kinyume cha sheria na kutumikishwa kama watumwa. Ripoti hiyo ambayo inazinduliwa leo siku ya kimataifa ya kutokomeza ajira kwa watoto inaitwa Kutokomeza ajira za watoto majumbani na inasema watoto zaidi ya Milioni Kumi duniani kote wamenaswa kwenye mtego huo. Kati yao hao Milioni Sita na Nusu wana umri wa kuanzia miaka Mitano hadi Kumi Nne, na wengi wao ni watoto wa kike. Mkurugenzi wa ILO anayeongoza mradi wa kutokomeza ajira kwa watoto, Dkt.Constance Thomas amesema ni nadra kwa watoto kuweza kujinasua kwenye mtego huo kwa kuwa wengi wao wanakuwa wanafanya kazi hizo kwa ujira mdogo na hata bila ujira kwa ndugu, jamaa au marafiki wa jamaa zao.   "Kazi ya nyumbani ni ajira, na watoto wanaoajiriwa majumbani ni ajira kwa watoto na inapaswa kuzuiwa, n...

MAZINGIRA MAGUMU YA SHULE KWA WALEMAVU…..

Image
                   MWANZONI mwa mwaka 2009,  mke wa Rais, Salma Kikwete aliitaka jamii kutowatenga wanafunzi wenye ulemavu badala yake wasaidiwe  na kushirikishwa  katika masuala mbalimbali ya kijamii ikiwemo kupewa elimu kama ilivyo kwa makundi mengine ya kijamii. Siku aliyotoa wito huo hakusita kusema kuwa zaidi ya Sh milioni 881 zinahitajika kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kusomea kwa wanafuzi 8700 wenye ulemavu nchini ili waweze kujifunza katika hali mazingira mazuri. Tunapozungumzia mazingira mazuri kwa wanafunzi wenye ulemavu hatumaanishi vifaa na mahitaji mengine ya kitaaluma pekee  bali hata miundombinu kama vyumba vya madarasa, vyoo, maktaba, maabara, mabweni na mazingira ya eneo zima la shule Kufanya hivi ni kuwapa fursa ya wao kujiona kuwa ni sehemu ya jamii hali itakayowapa ari ya kujifunza sambamba na wenzao wasiokuwa na ulemavu.   Mazingira ni miongoni mwa vitu vya ...

MAZINGIRA YA VYOO VYA SHULE MTIHANI KWA WALEMAVU

Image
Unapozungumzia mazingira mazuri kwa wanafunzi wenye ulemavu hatumaanishi vifaa na mahitaji mengine ya kitaaluma pekee  bali hata miundombinu kama vyumba vya madarasa, vyoo, maktaba, maabara, mabweni na mazingira ya eneo zima la shule Kufanya hivi ni kuwapa fursa ya wao kujiona kuwa ni sehemu ya jamii hali itakayowapa ari ya kujifunza sambamba na wenzao wasiokuwa na ulemavu. Hata hivyo, uchunguzi wangu mdogo umebaini kuwa pamoja na nia ya serikali kutaka watoto walemavu wapelekwe shule bado mazingira ya kujifunza katika shule nyingi hayawavutii watoto hawa hali inayosababisha baadhi yao kukacha masomo. Hivi leo serikali kupitia mipango kama MMEM, MMES na ujenzi wa shule za kata imefanikiwa kujenga shule nyingi kwa lengo la kutoa fursa zaidi kwa vijana wa Tanzania wanaopata elimu katika madaraja mbalimbali. Lakini ujenzi wa shule hizi umekuwa kikwazo kwa baadhi ya watoto kwa kuwa hali zao za kimaumbile zinawapa ugumu kurandana na hali ya mazingira ya shule. Peter...

NATAMANI SIKU MOJA KUWA RAIS WA NCHI YANGU, PAMOJA NA ULEMAVU NILIONAO: MWITA CHARLES

Image
Naitwa Mwita Charles kutoka katika wilaya ya Bunda, nina umri wa miaka 14. Nina wazazi wote wawili lakini baba anasumbuliwa na matatizo ya akili kwa sasa hivyo naishi na mama. Ninasoma shule ya msingi na niko katika   darasa la sita (6). Nina ulemavu wa viungo, nilizaliwa pasipokuwa na mikono yote miwili.                                     MWITA AKIANDIKA KWA KUTUMIA MGUU WAKE   Katika kusoma kwangu naandika kwa kutumia miguu. Jamii iliyo nizunguka inanichukulia kawaida, hawanitengi wala kuninyanyapaa, nacheza na kushirikiana na watoto wenzangu kama mtu wa kawaida. Mahusiano ya mama na baba sio mazuri kwasababu wakikutana wanaanza kupigana, baba anamkaba shingo mama kwasababu ya tatizo la akili alilonalo. Mama anafanya kazi ya vibarua, anahangaika sana ili kupata pesa ya kunitunza na kunisome...

MUNGU NDIYE MUUMBA NA ATAKAVYO PANGA HAKUNA ANAYEWEZA KUPANGUA. YOTE NI MAPENZI YAKE.!!!

Image
Watoto mapacha wa k iume wamezaliwa huko India wakiwa na vichwa viwili katika mwili mmoja kitu ambacho inasemekana ni nadra sana kutokea. Madaktari wamesema wanaamini wanauwezo wa kuokoa maisha ya watoto hao ambao wamezaliwa Jumatano (July 24) huko Jaipur, Rajasthan India. Kwa mujibu wa taarifa ya Daily Mail, nervous system ya watoto hao imetengana wakati uti wa mgongo umeungana na pia wanashare sehemu ya ubavu. Dr. S.D. Sharma, wa J.K. Lone Hospital amesema tatizo kama hilo ni nadra sana kutokea hususan kwa watoto wa kiume, na linafahamika kama ‘Dicephalic Parapagus’. Aliongeza kuwa tukio hilo ni la pili kutokea India. Daktari huyo aliendelea kusema kuwa mara nyingi watoto wenye ‘Dicephalic Parapagus’ huzaliwa wakiwa wamekufa, na mara nyingi hutokea kwa watoto wa kike. Kwa mujibu wa Sharma alisema kuna uwezekano wa kuokoa maisha ya mapacha hao.   Tatizo kama hilo lililowahi kutokea kwa mapacha wa kike kutoka Sudan mwaka (2011) ambao walioza...

HUU NI UNYAMA KWA WATOTO

Image
Moja kati ya ajira mbaya kwa watoto mkoani Iringa, huu mzigo ni mzito sana. Mtoto anatumikishwa kama myama Watoto wakazi wa Wangama wilaya ya Njombe mkoani Iringa ambao majina yao hayakuweza kupatikana mara moja wakikokota mkokoteni wa kuvutwa na wanyama ,wakielekea kubeba mahindi shambani kama walivyokutwa leo majira ya jioni, kwa kawaida mkokoteni huu hukokotwa na Ng'ombe au Punda ila kutokana na ugumu wa maisha watoto hawa wanajiingiza katika kazi ya namna hii. WITO KWA WANANCHI WOTE. Hata kama hatuwezi kuwasaidia watoto waishio kwenye  mazingira magumu bila kuwafanyisha kazi, ni vizuri tukaangalia hata kazi za kuwapa, hivi kweli huu ni ubinadamu kumpatia mtoto kazi zinazotakiwa kufanywa na gari au wanyama? HEAR MY VOICE inatoa wito kwa wanajamii kuwa na moyo wa huruma na hawa watoto kwani hawakupenda kuzaliwa katika hali waliyonayo.