Mungu ni mwaminifu sana. Hawa watoto ni walemavu wa akili wapo shule ya msingi Milongo ya jijini Mwanza, pamoja na ulemavu wao ila wana vipaji vya ajabu sana. Katika maisha yangu wameweza kuniondolea ule mtazamo kuwa walemavu hawawezi jambo lolote katika maisha Yao, huyo binti ana kipaji cha uimbaji, na hao vijana wana vipaji mbalimbali kama vile kucheza mpira yote hiyo ni katika kuutambua ukuu wa Mungu. Sio hao tuu kuna mifano mbalimbali ya Watu wenye ulemavu na wana vipaji mbalimbali mfano Voice wonder mwimbaji kipofu wa Marekani, Lena Maria. Dada mlemavu wa viungo wa Sweden mwimbaji mzuri sana na wengine wengi, hiyo ni mifano michache katika kuthibitisha kuwa ulemavu si kutokuweza.
AYA ZA BIBLIA KUHUSU WATU WENYE ULEMAVU
YOHANA 9:2-7 Wanafunzi wake wakamwuliza Wakisema Radi, ni yupi aliyetenda dhambi, mtu huyu au wazazi wake, hata zaliwe kipofu? Yesu akajibu, Huyu hakutenda dhambi wala wazazi wake; bali kazi za Mungu zidhihirishwe ndani yake. Imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenipeleka maadamu ni mchana na usiku waja asipoweza mtu kufanya kazi. Muda nilipo ulimwenguni mimi ni nuru ya ulimwengu. Alipokwisha kusema hayo alitema mate chini, akaifanya tope kwa yale mate. Akampaka kipofu tope za macho, akamwambia Nenda kanawe katika birika ya Siloamu, basi akaenda na kunawa; akarudi anaona. Basi jirani zake na wale waliomwona zamani kuwa ni mwombaji wakasema, Je! Huyu si Yule aliyekuwa akiketi na kuomba? Wengine wakasema, ndiye wengine wakasema La, lakini amefanana naye. Yeye mwenyewe alisema, Mimi ndiye. Mwandishi wa kitabu hiki amenikumbusha mbali, hasa kutokana na mitazamo hasi katika jamii dhidi ya walemavu kwa ujumla, ila pia nimepata amani hasa nili...
Comments
Post a Comment