SERIKALI INAYATAMBUA HAYA.?
Adha, shida na mateso wanayoyapata watoto katika maeneo ya machimbo ya dhahabu Chunya.
Mkazi
 wa kijiji cha Chang'ombe, Kata ya Mkwajuni jimbo la Songwe Mbuke Kulwa 
akitafuta dhahabu katika mto mara baada ya kufukuzwa na mumewe ambaye 
alidai kuwa anaishi na mke mwingine, huu ni sehemu ya ukatili wa Kijinsia
 ambao Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake TAMWA kimekuwa kikipinga 
na kukemea katika harakati zake za kupinga ukatili wa Kijinsia.
Kijana huyu Mwanafunzi wa shule ya Msingi Mkwajuni aliyejitambulisha 
kwa jina la  Asajile mkazi wa kitongoji cha Kamficheni Jimbo la Songwe 
Mkwajuni wilayani Chunya akitafuta dhahabu ili aweze kujikimu kutokana 
na mahitaji muhimu ya kila siku, Asajile ni miongoni mwa vijana wengi wa
 shule za Msingi ambao wamekuwa wakiacha masomo kwa na kwenda katika 
machimbo ya dhahabu wilayani Chunya.
Watoto hawa wakazi wa kitongoji cha Kigamboni kilichopo Jimbo la Songwe
 wilayani Chunya wakitafuta maji kwa ajili ya matumizi ya kila siku 
kutokana na uhaba wa maji katika mji huo,familia nyingi wilayani Chunya 
zimekuwa zikihangaika kusaka maji safi na salama kutokana na kukosekana 
mabomba ya maji kutosheleza kaya jimboni humo.
Mtoto
 huyu ambaye hakutambulika jina lake akiokota dhahabu ili kujipatia 
kipato kutokana na hali ngumu ya maisha yanayowakabili wakazi wa jimbo 
hilo.
Comments
Post a Comment