NI WAJIBU WETU.
 JAMII IWAJIBIKE KUWASAIDIA WATOTO WA MITAANI, YATIMA....           Kitanda usichokilalia, huwezi kujua  kunguni wake, shida na mateso wanayoyapata watoto waishio katika  mazingira hatarishi na wale wa mitaani ni vigumu kuyaeleza. Watoto hawa  hawajui leo au kesho watakula nini, hakuna anayehangaika kuwatafutia  chakula, wanapolala na njaa hakuna wa kumlilia na wakiumwa hakuna wa  kumweleza hivyo huendelea na maisha yao hadi wanapopata nafuu au kupona  kabisa.             Ukweli ni kwamba, watoto hawa  hujisikia wapweke kutokana na jamii kubwa kuwakataa na kuwaweka katika  fungu tofauti. Jambo la kusikitisha ni idadi kubwa ya watoto hawa umri wao  unaanzia miaka miwili hadi kumi ambao kimsingi hawajui kujitegemea, njaa  ikiuma wanalia tu na kushindwa kujieleza. Kitanda chao ni barabarani na  wengine mitaroni, baridi yote ya usiku na jua la mchana ni lao ,hawajui  kubadilisha nguo, zile walizovaa wiki iliyopita hadi leo hazijatoka  mwilini,  Tumezo...
