 Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi 
na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akimsikiliza kwa 
makini Mkuu wa kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija 
Jumuishi ya mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi aliyekuwa akimwelezea 
changamoto mbalimbali walizonazo shuleni hapo.(Picha na Zainul Mzige).
Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi 
na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akimsikiliza kwa 
makini Mkuu wa kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija 
Jumuishi ya mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi aliyekuwa akimwelezea 
changamoto mbalimbali walizonazo shuleni hapo.(Picha na Zainul Mzige). 
Na MOblog, Shinyanga
SHULE
 ya watoto wenye ulemavu ya Buhangija Jumuishi inakabiliwa na changamoto
 kubwa zinazofanya maisha kwa watoto hao kuwa magumu.
Miongoni mwa changamoto hizo ni kukosekana kwa huduma za matibabu, walimu wa kutosha na mabweni.
Hayo 
yamebainika wakati wa ziara fupi ya Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja
 wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) 
Tanzania, Zulmira Rodrigues.
Mkuu 
wa Kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi 
iliyopo mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi, ndiye aliyeelezea ugumu 
uliopo katika shule hiyo yenye wanafunzi 209 wenye ulemavu wa aina 
mbalimbali.
 Mkuu
 wa kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya 
mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi akimtambulisha Mkurugenzi Mkazi wa 
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na 
Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues aliyefanyia ziara fupi 
akiwa safarini kuelekea jijini Mwanza akiwa ameambatana na Afisa Mradi 
wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias 
(katikati).
Mkuu
 wa kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya 
mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi akimtambulisha Mkurugenzi Mkazi wa 
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na 
Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues aliyefanyia ziara fupi 
akiwa safarini kuelekea jijini Mwanza akiwa ameambatana na Afisa Mradi 
wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias 
(katikati). 
Alisema
 shule hiyo yenye walemavu wa aina tatu wa kusikia, ngozi na wasioona 
inakabiliwa pia na lishe duni ambayo haimpi kijana nafasi ya kuendelea, 
kwani wanakula mlo wa aina moja na kidogo.
Shule
 hiyo ambayo awali ilikuwa inawapokea wanafunzi wasioona sasa inapokea 
walemavu wa ngozi kutokana na hofu iliyokuwa inalikumba taifa ya mauaji 
ya albino.
Aidha
 mwalimu huyo alisema kwamba wameiomba serikali kuwa na muuguzi na 
daktari katika makazi hayo lakini mpaka sasa hawajapatiwa kutokana na 
wao wenyewe kutokuwa na uwezo wa kuwalipa.
Alisema
 kutokana na rika mbalimbali na tatizo la walemavu wa ngozi shule hiyo 
ambayo sasa imegeuzwa kuwa makazi inastahili kuwa na daktari na mabweni 
yaongezwe.
 Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi 
na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues ( wa pili kushoto) 
akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani
 Shinyanga (hawapo pichani) alipofanya ziara fupi akiwa safarini 
kuelekea jijini Mwanza akiwa ameambatana na Afisa Mradi wa Elimu ya Afya
 na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias (wa pili kulia). Kulia 
ni Mkuu wa kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija 
Jumuishi ya mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi.
Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi 
na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues ( wa pili kushoto) 
akizungumza na wanafunzi wa shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani
 Shinyanga (hawapo pichani) alipofanya ziara fupi akiwa safarini 
kuelekea jijini Mwanza akiwa ameambatana na Afisa Mradi wa Elimu ya Afya
 na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias (wa pili kulia). Kulia 
ni Mkuu wa kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija 
Jumuishi ya mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi. 
Aidha mwalimu alisema walimu kwa ajili ya viziwi hawatoshi.
Naye 
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu,
 Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues, amesema 
ameyaona mazingira hayo na kuahidi kushirikiana na marafiki na mamlaka 
nyingine kuboresha mazingira ya kituo hicho.
Alisema
 kwamba amefurahishwa kuwapo katika kituo hicho na kuona namna 
wanavyoweza kusaidia sehemu hiyo ya jamii kutojisikia upweke.
Akizungumza
 na watoto hao walimwambia kwamba wana changamoto ya nguo, vitanda, 
vitabu na mahitaji mengine ya lazima kama watoto na wanafunzi.
 Baadhi
 ya watoto wanaosoma shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani 
Shinyanga wakimsikiliza Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa 
linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira
 Rodrigues (hayupo pichani).
Baadhi
 ya watoto wanaosoma shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani 
Shinyanga wakimsikiliza Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa 
linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira
 Rodrigues (hayupo pichani). 
 Mwanafunzi
 wa kidato cha pili shule ya sekondari Loreto mkoani Shinyanga Beatrice 
Leme anayelelewa kwenye kituo hicho kutokana na kukithiri kwa mauaji ya 
walemavu wa ngozi mkoani humo akimwelezea changamoto mbalimbali 
zinazowakabili kwa niaba ya wanafunzi wenzake Mkurugenzi Mkazi wa 
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na 
Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues aliyefanya ziara fupi 
shuleni hapo.
Mwanafunzi
 wa kidato cha pili shule ya sekondari Loreto mkoani Shinyanga Beatrice 
Leme anayelelewa kwenye kituo hicho kutokana na kukithiri kwa mauaji ya 
walemavu wa ngozi mkoani humo akimwelezea changamoto mbalimbali 
zinazowakabili kwa niaba ya wanafunzi wenzake Mkurugenzi Mkazi wa 
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na 
Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues aliyefanya ziara fupi 
shuleni hapo. 
 Mwanafunzi
 wa darasa la sita shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani 
Shinyanga, Daniel Limbu akizungumza na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la 
Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) 
Tanzania, Zulmira Rodrigues kwa niaba ya wanafunzi wenzake.
Mwanafunzi
 wa darasa la sita shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya mkoani 
Shinyanga, Daniel Limbu akizungumza na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la 
Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) 
Tanzania, Zulmira Rodrigues kwa niaba ya wanafunzi wenzake. 
 Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi 
na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues, Afisa Mradi wa Elimu 
ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias pamoja na Mkuu 
wa Kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya 
mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi wakifurahi pamoja na watoto wenye 
ulemavu wa ngozi katika shule hiyo.
Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi 
na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues, Afisa Mradi wa Elimu 
ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias pamoja na Mkuu 
wa Kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi ya 
mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi wakifurahi pamoja na watoto wenye 
ulemavu wa ngozi katika shule hiyo. 
 Afisa
 Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias 
katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto wenye ulemavu wa ngozi 
wanaolelewa kwenye kituo hicho ambacho ni salama kwao kutokana na hofu 
iliyokuwa inalikumba taifa ya mauaji ya albino.
Afisa
 Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias 
katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto wenye ulemavu wa ngozi 
wanaolelewa kwenye kituo hicho ambacho ni salama kwao kutokana na hofu 
iliyokuwa inalikumba taifa ya mauaji ya albino. 
 Baadhi ya majengo ya mabweni ya shule ya msingi Buhangija ya wilayani Shinyanga.
Baadhi ya majengo ya mabweni ya shule ya msingi Buhangija ya wilayani Shinyanga. 
 Baadhi
 ya watoto wenye ulemavu wa ngozi wakicheza mpira kwenye mazingira 
salama shuleni hapo kutokana na hofu iliyokuwa inalikumba taifa ya 
mauaji ya albino.
Baadhi
 ya watoto wenye ulemavu wa ngozi wakicheza mpira kwenye mazingira 
salama shuleni hapo kutokana na hofu iliyokuwa inalikumba taifa ya 
mauaji ya albino. 
 Mkuu
 wa Kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi 
iliyopo mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi akimtambulisha mtoto Erick 
mwenye ulemavu wa ngozi kwa Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa 
Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania,
 Zulmira Rodrigues (kushoto) aliyefanya ziara fupi kwenye kituo cha 
kulelea watoto wenye ulemavu (mahitaji maalum).
Mkuu
 wa Kitengo cha watoto walemavu shule ya msingi Buhangija Jumuishi 
iliyopo mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi akimtambulisha mtoto Erick 
mwenye ulemavu wa ngozi kwa Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa 
Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania,
 Zulmira Rodrigues (kushoto) aliyefanya ziara fupi kwenye kituo cha 
kulelea watoto wenye ulemavu (mahitaji maalum). 
 Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi 
na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akimsuka kwenye bembea
 mmoja wa watoto wenye ulemavu wa ngozi Zawadi Deus anayesoma shule ya 
msingi Buhangija Jumuishi iliyopo mkoani Shinyanga wakati wa michezo 
alipofanya ziara fupi shuleni hapo.
Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi 
na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akimsuka kwenye bembea
 mmoja wa watoto wenye ulemavu wa ngozi Zawadi Deus anayesoma shule ya 
msingi Buhangija Jumuishi iliyopo mkoani Shinyanga wakati wa michezo 
alipofanya ziara fupi shuleni hapo. 
 Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi 
na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akisaini kitabu cha 
wageni wakati akijiandaa kuondoka shuleni hapo baada ya kuhitimisha 
ziara yake fupi. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha watoto walemavu shule ya 
msingi Buhangija Jumuishi iliyopo mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi.
Mkurugenzi
 Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi 
na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akisaini kitabu cha 
wageni wakati akijiandaa kuondoka shuleni hapo baada ya kuhitimisha 
ziara yake fupi. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha watoto walemavu shule ya 
msingi Buhangija Jumuishi iliyopo mkoani Shinyanga Mwl. Loyce Daudi. 
 
Comments
Post a Comment