KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA WALEMAVU KITAIFA IRINGA , SERIKALI YA TANZANIA YAPIGA MARUFUKU UJENZI WA MAJENGO YASIYO RAFIKI NA WALEMAVU.
 SERIKALI  imeziagiza  mamlaka  za 
usafiri  wa majini na nchi kavu (SUMATRA )  nchini  kuanza
mchakato  wa  kukaa na  wamiliki wa  vyombo 
hivyo  ili kuanza  uangizaji  wa vyombo  vya usafiri
yakiwemo mabasi ambayo ni  rafiki na walemavu nchini huku ikipiga
marufuku  majengo ya   serikali kujengwa bila kuwepo kwa 
mchoro  unaoonyesha mazingira yanayozingatia makundi  yote ya
jamii  likiwemo la walemavu wa viungo .
Agizo   hilo  limetolewa na  waziri 
mkuu Mizengo  Pinda wakati  wa maadhimisho ya  siku ya 
walemavu  duniani yaliyofanyika   kitaifa  katika 
viwanja  vya kichangani mkoani  Iringa jana.
Akiwahutubia   walemavu hao na  wananchi 
waliofika katika  viwanja   hivyo waziri  mkuu
,aliyewakilishwa na waziri  wa nchi  ofisi ya  waziri mkuu (sera
na uratibu wa bunge)  ,Wiliam Lukuvi ambae ni mbunge wa  jimbo la
Isimani mkoani Iringa alisema  kuwa  kimekuwepo kilio  cha
muda  mwingi  kutoka kwa  walemavu  juu ya kusaulika katika
ujenzi  wa  majengo mbali mbali ambayo yamekuwa 
yakijengwa  bila kuzingatia  kundi la  watu  wenye 
ulemavu jambo ambalo ni sawa na  kuwabagua watu  hao.
Hivyo  alisema  katika  kuona kilio 
hicho  cha  walemavu  kinafanyiwa  kazi  kuanzia 
sasa majengo  yote ya  serikali  zikiwemo  shule na taasisi
nyingine  kabla ya  kuanza  ujenzi  wake lazima 
wasimamizi wa  ujenzi  huo kujiridhisha kwa  mchoro ambao 
utaonyesha  mazingira  yatakayomuwezesha  mlemavu  
kutumia jingo  hilo bila usumbufu  tofauti na  ilivyo sasa
ambapo  idadi kubwa ya majengo mazingira  yake  si lafiki
kwa  walemavu.
"  Ni  siku  nyingi  watu  wenye
ulemavu  wamekuwa  wakilalamika juu ya mazingira  yasiyo
rafiki    katika majengo  mbali mbali .....sasa  leo
naomba  kuagiza  kuwa michoro yote inayochorwa katika majengo
ya  huduma za  kijamii  ni marufuku  kupitishwa ama 
wasimamizi  wa  ujenzi  husika  kuruhusu ujenzi  iwapo
mchoro hauonyeshi  kama utayajali makundi  yote wakiwemo 
walemavu.....wasimamizi  wote msikubali  kusimamia  wala 
kutangaza  tenda  ya ujenzi kama ramani  yake  si rafiki
kwa  walemavu.....lakini  pia  hata  kwenye mabasi hivi
unamtegemea mtu mwenye ulemavu wa miguu ataingia vipi na baiskeli 
yake  katika gari iwapo hakuna mazingira  yanayomwezesha 
kuingia .... hivi  sasa  teknlojia  imezidi kukua na baadhi ya
nchi  wameanza muda mrefu kuwajali walemavu kwa kuwa na mabasi ambayo
mlemavu anaingia na baiskeli  yake  na  kushuka nayo  
bila usumbufu ni vema hata Sumatra kuangalia uwezekano wa  kuwajali 
walemavu hao . pia ni vizuri  hata nyumba  za  ibada  nazo
ningeshauri baba askofu   kuangalia kuweka mazingira "
alisema  Lukuvi.
Kuhusu  ombi la walemavu hao   hasa 
wale  wasio sikia kuomba  serikali  kuwa na wakalimani katika
kituo cha Televisheni ya  Taifa (TBC) na vituo  vingine 
vya  luninga  ili  kuwawezesha  walemavu hao nao  kuweza 
kufuatilia hotuba  ya Rais mwisho  wa mwezi na mambo mengine badala
ya  kutengwa ,alisema  kuwa  suala  hilo 
ni  wajibu wa  serikali  kuwajali  watu  wake 
hivyo tayari  imeuagiza  uongozi  wa TBC na mamlaka ya 
mawasiliano Tanzania (TCRA)  kulitafutia  ufumbuzi  suala 
hilo la  mkalimani  hasa katika TBC .
Katika  hatua nyingine  Lukuvi  aliwataka 
walemavu hao  ili  ombi lao la  kutazamwa katika  nafasi
za  uongozi  liweze  kuzingatiwa ni  vema  wao 
wenyewe  kujitokeza kwa  wingi  kuipigia  kura 
katiba  iliyopendekezwa pindi  itakapokuja kwa  wananchi kwa
madai kuwa  katika  katiba   hiyo imezingatia mambo 
mengi ya kijamii likiwemo la  kuwajali  watu  wenye ulemavu
kwa  kuwatengea nafasi nyingi  zaidi  na  iwapo 
katiba  hiyo  itapitishwa kazi ya msuguano wa  rushwa
unaweza  kuhamia kwa  walemavu kwa kila mmoja kutaka  kupewa
nafasi.
" Hadi  hivi  sasa ni chama cha mapinduzi (CCM)
pekee ambacho  kina wabunge wa viti maalum wa  kuteuliwa  kutoka
kundi la  walemavu huku  vyama  vingine  vyote  havijawakumbuka
kabisa  watu  wenye ulemavu ukiacha  mbunge wa  jimbo la
Lindi mjini pekee ambae hakupendelewa  katika ubunge  wake bali
alishindwa kihalali kwa  kuchaguliwa na  wananchi 
wake..nafikiri  tushirikiane  kuhakikisha katiba  hii
iliyopendekezwa  inapita  ili  tuungane pamoja katika 
kujenga nchi  yetu "
Katika  salam  za  walemavu waziri  wa
Afya  na ustawi  wa jamii  Dkt Seil S. Rashid  zilizotolewa
kwa  niaba  yake  na mwenyekiti  wa baraza la 
watu  wenye ulemavu nchini na Dunford Makala   alisema 
kuwa  wizara  inaendelea   kuimarisha  ushirikiano na
vyama  vya  watu wenye ulemavu  na  shirikiasho  la
vyama  vya  watu  wenye ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA)
katika  kuhakikisha utekelezaji  wa uwekaji  wa fursa  na
haki  sawa  kwa  watu  wenye ulemavu nchini .
Alisema  katika  kuhakikisha ushirikiano
unakuwepo  wizara yake  imezindua baraza  la  ushauri 
la Taifa  la  watu  wenye  ulemavu  toka mnamo 1 
Novemba 2014 na katika  hilo  kamwe  hawataacha 
kumpongeza  Rais Dkt Jakaya Kikwete  kwa   kumteua 
mwenyekiti  wa baraza hilo
Aidha  alisema  kuwa ni ukweli  usiopingika kuwa
nchi  hii chini ya Rais Dkt  Kikwete  imefanya mambo 
mengi  zaidi ya  kuwajali  watu  wenye  ulemavu 
katika Nyanja  za  kiuchumi ,kiutamaduni na  kisiasa
ambavyo  vyote  hivyo  kumwezesha  mlemavu kujikwamua 
kimaisha
Hata   hivyo  alisema  ushahidi  wa
yote hayo ni pamoja na kuridhia mikataba  ya kimataifa  juu ya
haki  za watu wenye ulemavu , kutungwa kwa sharia Na.9 ya mwaka 2010 ya
watu  wenye ulemavu  na kanuni zake ,kuwashirikisha  watu wenye
ulemavu  katika tume ya mabadiliko ya katiba  ya Jamhuri ya 
muungano wa Tanzania pamoja na kuteuliwa kwa  wajumbe 20  wenye
ulemavu  katika  bunge maalumu la mabadiliko ya katiba la mwaka 2014.
Awali  walemavu hao  katika  risala yao 
iliyosomwa na makamu  mwenyekiti  wa SHIVYAWATA  Amina
Mollel  pamoja na  kuishukuru  serikali kwa jinsi 
kwa  kuendelea  kuwa karibu  zaidi na  watu  wenye
ulemavu kwa kushiriki shughuli mbali mbali za  walemavu ,bado
waliweza  kuishukuru  serikali kwa kuandaa sera ya maendeleo ya 
watu wenye ulemavu ya mwaka 2004, kutambuliwa  kwa  watu wenye
ulemavu katika MKUKUTA,kuwezesha kuongezeka kwa idadi ya watu wenye
ulemavu  wanaopata  elimu kuanzia shule za msingi hadi elimu ya juu
na mambo  mengine  mengi ambayo  wao kama  walemavu
wamekuwa  wakiona  serikali  yao  ipo pamoja nao.
Sanjari na mema  hayo bado  waliiomba serikali
kuzingatia kuwapatia  walemavu mambo muhimu katika maisha ya kila 
siku ikiwa ni pamoja na kuwa na vyombo  vya usafiri rafiki kama
magari  moshi.vyombo  vya usafiri majini ,angani ,miundo mbinu katika
 majengo  na viwanja  vya  ndege ambavyo  vitamwezesha
mlemavu pia kuwa  huru .
Mkuu  wa mkoa wa Iringa Amina Masenza  alisema 
kuwa maadhimisho hayo yaliyofanyika  chini ya kauli  mbiu 
isemayo " Maendeleo endelevu ;Ahadi  ya Teknolojia  huku
mkoa  wa  Iringa  ukiendelea  kuwa  bega kwa 
bega  na  walemavu ikiwa ni pamoja na  kufanya kazi karibu
na  vyama  hivyo  vya  watu  wenye 
ulemavu   na kuwa mkoa huo  kwa  sasa una jumla ya 
walemavu  zaidi ya 179 ,000 na  wote  serikali 
imeendelea  kuwalinda na  kuwa nao pamoja.
Comments
Post a Comment