SIKU YA MTOTO WA AFRIKA
    Siku ya Mtoto wa Afrika na Elimu bora isiyo vikwazo              Mtoto akitafakari   Juni 16 ya kila mwaka Umoja wa Afrika sambamba na washirika  wake  husherekea siku ya mtoto wa Afrika- au kwa kimombo Day of African Child  (DAC ), ikiwa ni kumbukumbu ya mwaka 1976 ambapo waandamanaji wanafunzi  wa shule za Soweto Afrika ya Kusini waliandamana kupinga elimu iliyokuwa  inatolewa kwa manufaa ya utawala wa kibaguzi wa makaburu. Maandamano  hayo yalipokelewa na mikono usio na huruma na masikio yasiyo sikivu ya  utawala wa kibaguzi na kusababisha vifo vya mamia ya wanafunzi    “Watu wangu, leo nipo huru nipo huru kwa kuwa sintosahaulika kabisa,  siku itatimia ambapo kila mmoja wetu atakuwa huru, huru kutokana na  unyanyasaji, huru kutokana na uwoga, huru kutokana na kuuwawa, nyinyi ni  vijana wadogo mtaishi hadi kuiona siku hiyo na ata kama sintofanikiwa  kuiona siku hiyo nyinyi mnatakiwa kusadiki tu kuwa nitakuwepo siku hiyo,  hapa ni nyumbani kwangu, pahala pangu pa kuishi.” Hayo ni ...