HILI NI LA KUANGALIA KWA JICHO LA PEKEE....
     Tanzania ina shule moja tu ya sekondari ya viziwi!                Kaimu  Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Elimu Maalumu kutoka Wizara ya Elimu na  Mafunzo ya Ufindi Estrida Kimweri akieleza changamoto ya kuwa na shule  moja ya sekondari kwa walemavu viziwi.   Tanzania inakabiliwa na changamoto ya kuwa na shule moja ya sekondari  kwa walemavu wasiosikia, toka ipate uhuru, hii haiendani na sheria ya  mwaka 2010 ya walemavu ambayo inatetea kundi hilo kupata elimu.   Akizungumza katika mahojiano maalum na Taarifanews.com Kaimu  Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Elimu Maalumu kutoka Wizara ya Elimu na  Mafunzo ya Ufundi Estrida Kimweri, changamoto hiyo inapelekea kukosa  idadi kubwa ya walemavu wa aina hiyo wanaomaliza mpaka shule ya  sekondari.   Kimweri alisema kuwa shule hiyo ipo mkoa wa Njombe na kuna wanafunzi  wengi sana wanaoletwa kutoka katika shule mbalimbali, kupata elimu ya  sekondari kwenye shule hiyo, lakini nafasi yake ni ndogo sana kuweza  kupokea wanafunzi wengi.   Kwa sas...